TRC yatoa ufafanuzi kuhusu ajali iliyohusisha treni ya kisasa ya EMU

DAR-Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa taarifa rasmi kuhusu ajali iliyohusisha treni ya kisasa ya EMU iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma, majira ya saa 2:00 asubuhi ya leo Oktoba 23, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ajali hiyo imetokea katika kituo cha Ruvu na imetokana na hitilafu za kiuendeshaji. Hata hivyo, taarifa za awali zinaeleza kuwa hakuna tukio la kifo lililoripotiwa kufuatia ajali hiyo.

TRC imeeleza kuwa tayari timu ya wataalamu imeanza uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo. Timu hiyo inaongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mkurugenzi Mkuu wa TRC, pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama na menejimenti ya TRC.

Aidha,shirika limewahakikishia wananchi kuwa juhudi zinaendelea kufanyika ili kurejesha huduma kwa haraka na kuhakikisha usalama wa abiria unaendelea kupewa kipaumbele.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news