Wanarufiji tumpe kura za kutosha Rais Dkt.Samia-Mchengerwa

NA YOHANA KIDAGA

MGOMBEA wa Ubunge jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa amesema endapo wananchi watampa ridhaa ya kumchagua tena katika kipindi hiki atakwenda kusimamia maendeleo ya wananchi wa Jimbo hili, huku akimwombea kura Mhe Rais Samia.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi katika Kata ya Kipugira Mhe. Mchengerwa amesema katika kata hilo endapo atachaguliwa atakwenda kuishawishi Serikali kukamilisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mloka hadi Mkongo ili ipitike katika kipindi chote cha mwaka.

"Naomba niwahakikishie miaka mitano ijayo tutapambana kufa na kupona kuhakikisha kuwa barabara ya Mloka hadi Mkongo inakwenda kujengwa kwa kiwango cha lami.Najua hiki ndiyo kilio kikubwa cha Tarafa ya Mkongo".
Amesisitiza Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa huku akishangiliwa na wananchi wakionyesha kuwa anatambua vema changamoto ya Wanakilugila na Rufiji kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa siasa zake ni za maendeleo ya kwa maana ya kwamba siasa zake zimelenga katika kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli na siyo ujanja ujanja.

Aidha, amewahimiza wanananchi kufanya kazi kwa bidiii ili kuondokana na umasikini na kuinua hali zao za maisha huku akisisitiza kuwa maendeleo huletwa kwa kufanya kazi.

Mheshimiwa Mchengerwa ametumia mkutano huo kutaja mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi chote cha miaka kumi cha mabadiliko ya fikra kwa wananchi wa Rufiji.
Baadhi ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi hicho ni pamoja na ongezeko kubwa la ujenzi wa miundombinu inayojumuisha madaraja barabara na taa za barabarani, shule za msingi na Sekondari, vituo vya afya na hospitali pia huduma za maji na umeme katika vijiji vyote 38 vya Jimbo hilo.

Leo Mheshimiwa Mchengerwa anaendelea na mikutano ya hadhara katika kata nyingine za Jimbo hilo kuomba kura kwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa madiwani na kwake mwenyewe ili apewe ridhaa ya kuwaongoza tena katika kipindi hiki.

Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa ni Mbunge wa tisa wa kuchaguliwa katika jimbo hilo la Rufiji toka lianzishwe na kuongozwa na wabunge kadhaa kuanzia Mhe. Bibi Titi Mohamed ambapo anaelezewa kuwa ni miongoni mwa wabunge walioliletea maendeleo makubwa Jimbo hilo ukilinganisha na wabunge waliotangulia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news