DCEA yawaelimisha wafanyakazi 101 wa Uwanja wa Ndege Songwe na Iringa kuhusu mbinu mpya za wasafirishaji wa dawa za kulevya

SONGWE-Katika kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini, Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imeendelea kutoa elimu kwa wadau muhimu wanaoshiriki moja kwa moja katika kuhakikisha usalama wa mipaka na safari za anga.
Elimu hii imetolewa kwa maafisa, wahudumu na wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Songwe (Mbeya) pamoja na Uwanja wa Ndege wa Iringa.
Jumla ya wahudumu 101 wamepatiwa elimu inayohusu tatizo la dawa za kulevya, ikijumuisha mbinu za kisasa za ufichaji wa dawa (concealment methods) zinazotumiwa na wasafirishaji kupitia viwanja vya ndege, pamoja na dalili na viashiria muhimu vya kuwatambua watu wanaoweza kujihusisha na biashara au usafirishaji wa dawa za kulevya.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news