Magazeti leo Novemba 22,2025

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Vision Care ya Korea Kusini imefanikiwa kuwafanyia upasuaji watu 60 waliohitaji huduma ya upasuaji wa mtoto wa jicho kwa njia ya tundu dogo kupitia kambi maalum ya siku tano iliyoanza tarehe 17 Novemba 2025 na kuhitimishwa tarehe Novemba 21, 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhitimisha kambi hiyo Novemba 21, 2025, Mkuu wa Idara ya Macho wa MNH, Dkt. Joachim Kilemile, amesema kuwa kambi hiyo imekuwa na mwitikio mkubwa na imefanikisha kutoa huduma bora kwa wagonjwa waliokuwa wakisubiria kupata huduma hiyo muhimu.

“Takwimu zinaonyesha kuwa mtoto wa jicho ni miongoni mwa changamoto kubwa za kiafya nchini, na husababisha takribani asilimia 20 ya upofu Tanzania. Kati ya wagonjwa 24 wanaofika hospitalini wakiwa vipofu, karibu 19 hupatikana kuwa na tatizo hili, jambo linaloonyesha ukubwa wa hitaji la huduma za matibabu ya mtoto wa jicho,”amesema Dkt. Kilemile.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news