Magazeti leo Novemba 5,2025

KIJANA kutoka Shinyanga Mjini, Peter Alex Frank, maarufu kwa jina la Mr. Black, amejitosa rasmi kuwania nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mr. Black amechukua na kurejesha fomu Novemba 4, 2025, katika Makao Makuu ya CCM Taifa, Dodoma, hatua inayomweka kwenye orodha ya watia nia wanaowania nafasi hiyo muhimu ya uongozi wa chombo cha kutunga sheria nchini.

Akiwa kijana pekee miongoni mwa watia nia waliorejesha fomu hadi sasa, Mr. Black amesema uamuzi wake unatokana na dhamira ya dhati ya kutumia uwezo alio nao katika kulinda na kusimamia kanuni, sheria na taratibu za Bunge, pamoja na kuhamasisha utendaji na uchapakazi wa wabunge katika majimbo yao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news