Rais Mnangagwa ampongeza Rais Dkt.Samia kwa ushindi mkubwa uchaguzi mkuu

HARARE-Rais wa Zimbabwe, Mheshimiwa Emmerson Mnangagwa amemtumia salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia ushindi wake mkubwa katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 29,2025.
Katika taarifa yake, Rais Mnangagwa amesema, ushindi wa Rais Samia unaonesha imani na ujasiri wa wananchi wa Tanzania katika uongozi wake pevu na sera za chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Rais Mnangagwa amesisitiza ahadi ya Zimbabwe kuendelea kushirikiana kwa karibu na Tanzania ili kuimarisha na kupanua uhusiano mzuri wa urafiki na mshikamano kati ya mataifa na wananchi wa nchi hizo mbili.

Uchaguzi wa Tanzania ulimalizika hivi karibuni kwa ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news