Waziri Mkuu mteule Dkt.Mwigulu Lameck Nchemba kuapishwa kesho

Taarifa ya Ikulu imesema kuwa hafla ya uapisho itafanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma kuanzia saa 10:00 asubuhi.

Uteuzi wa Dkt. Mwigulu umefanyika baada ya jina lake kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Novemba 13, 2025.

Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Mwigulu alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango. Anachukua nafasi ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ambaye amehitimisha kipindi cha miaka 10 cha utumishi wake kama Waziri Mkuu.

Hafla hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wabunge, pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news