Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mheshimiwa Mobhare Matinyi, akisalimiana na Mfalme Carl XVI Gustaf wa Sweden, kwenye Kasri la Mfalme jijini Stockholm, tarehe 9 Desemba, 2025. Kushoto ni Binti Mrithi wa Ufalme, Victoria, katikati ni Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Sweden, Balozi Maria Christina Lundqvist, na kulia ni Mke wa Balozi, Yvonne Matinyi. Katika mazungumzo yao mafupi, Mfalme Gustaf na Balozi Matinyi walijadiliana kuhusu uimarishaji wa uhusiano baina ya nchi hizo mbili, hususani, katika nyanja za biashara, uwekezaji na utalii. (Picha kwa hisani ya Kasri la Mfalme).
