Wazazi na vijana Singida wapewa elimu ya matumizi salama ya mitandao ya kijamii

SINGIDA-Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida kupitia Dawati la Jinsia na Watoto, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, limetoa elimu ya matumizi salama ya mitandao kwa wazazi na vijana ili kuwalinda dhidi ya ukatili wa kijinsia wa kidijitali. Elimu hiyo ilitolewa Novemba 27, 2025, katika Hospitali ya Wilaya ya Singida ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia Duniani.

Mkuu wa Dawati la Jinsia ASP Theresia Mdendemi akishirikiana na Inspekta Amina Fakhi waliwaeleza wazazi na vijana namna bora ya kutumia mitandao bila kuingia kwenye hatari, ikiwemo kutowasiliana na watu wasiojulikana, kutambua vitendo vya udhalilishaji na kuweka mipaka ya matumizi ya simu kwa watoto.
Pia walieleza aina za ukatili, athari zake na umuhimu wa kutoa taarifa mapema.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Abel Zabroni aliwashukuru kwa elimu hiyo na kuahidi kushirikiana na Jeshi la Polisi kuwaunganisha waathirika wa ukatili na vyombo vya usalama ili kusaidia upatikanaji wa msaada wa kisheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news