Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yaonya dhidi ya utapeli wa uwekezaji mtandaoni

DODOMA-Benki Kuu ya Tanzania inatoa tahadhari kwa umma kufuatia kuongezeka kwa matangazo na machapisho ya mtandaoni yanayohusisha utapeli wa uwekezaji, yakiwemo yanayotumia picha au video bandia zinazotengenezwa kwa teknolojia ya Akili Unde (AI) na kudai ushiriki wa viongozi wa serikali au watu maarufu.
Wananchi wanahimizwa kuepuka kufungua viungo visivyoeleweka, kutoa taarifa binafsi au kutuma fedha kwa majukwaa yasiyothibitishwa, na kuhakikisha fursa zozote za uwekezaji zinathibitishwa na mamlaka husika kama Benki Kuu ya Tanzania au CMSA, huku matangazo yanayotiliwa shaka yakitakiwa kuripotiwa kwa mamlaka zinazohusika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here