Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga atembelea banda la DIB katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, akipata maelezo kutoka kwa Mwanasheria wa Bodi ya Bima ya Amana (DIB), Bi. Esther Mpendaamani kuhusu majukumu ya DIB wakati alipotembelea banda la DIB katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Usagara jijini Tanga tarehe 21 Januari 2026.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, akielezea kufurahishwa na maelezo kuhusu majukumu ya DIB na namna taasisi hiyo inavyowaelimisha wananchi jinsi inavyokinga amana zao katika benki na taasisi za fedha wakati alipotembelea banda la Bodi ya Bima ya Amana katika Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Usagara jijini Tanga.
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa Umma na Mawasiliano wa DIB, Lwaga Mwambande akifafanua jambo kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa Umma na Mawasiliano wa DIB,Bw.Lwaga Mwambande wakati alipotembelea banda la bodi hiyo na kupata maelezo kuhusu shughuli zake tarehe 21 Januari 2026.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here