Magazeti leo Januari 16,2026

Hatua kubwa ya mageuzi ya kodi nchini imefikiwa kufuatia tangazo la kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa ukusanyaji wa kodi za ndani, hatua inayotarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya mapato ya Serikali.
Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),CPA Yusuph Mwenda, amesema mfumo huo utaanza rasmi kutumika Februari 9, 2026, baada ya Serikali kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni 100 katika ujenzi na uboreshaji wa mifumo ya kisasa ya ukusanyaji wa kodi.

CPA Mwenda amesema mfumo huo umeundwa kwa kuzingatia changamoto na malalamiko ya muda mrefu yaliyokuwa yakikabili walipa kodi, hususan katika masuala ya urahisi wa ulipaji, ufanisi wa huduma na uwazi katika makadirio na ukusanyaji wa kodi za ndani.

Ameeleza kuwa kupitia mfumo huo mpya, TRA inalenga kuongeza uwazi na uwajibikaji, kupunguza mwingiliano wa moja kwa moja kati ya mlipa kodi na mtumishi wa umma, pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika kusimamia mapato ya Serikali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here