Maonesho ya 12 ya Biashara yazinduliwa Zanzibar,TMA yashiriki kikamilifu

ZANZIBAR-Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amezindua rasmi Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara Zanzibar (ZITF) katika viwanja vya Nyamanzi Januari 7, 2026.
Ameeleza kuwa, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji na wafanyabiashara, huku akisisitiza umuhimu wa sekta binafsi katika kufanikisha maendeleo endelevu ya taifa.
Katika hafla hiyo, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) iliwakilishwa na Mkurugenzi wa TMA ofisi ya Zanzibar, Masoud Makame Faki, ambaye aliwakumbusha wananchi kutembelea banda la TMA ili kupata elimu ya sayansi ya hali ya hewa, hususan katika kipindi hichi ambacho dunia inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi, ambapo mifumo ya hali ya hewa imekuwa ikibadilika mara kwa mara na kusababisha athari kwa sekta mbali mbali za uchumi na kijamii.

Hivyo basi matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa ni suluhisho mbadala kwa ajili ya kukuza uchumi na biashara katika sekta tofauti zikiwemo kilimo, uvuvi, viwanda, nishati, ujenzi, mawasiliano nakadhalika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here