Tafakari ya Maisha:Ufahamu umri wako na kusudi la kuishi

NA DIRAMAKINI

KATIKA safari ya maisha, binadamu mara nyingi husahau jambo moja la msingi, kwamba muda hauchelewi kwa mtu yeyote.
Picha na ZE.

Kadri siku zinavyopita, umri husonga mbele bila kusita, na kila hatua ya maisha hubeba wajibu, tafakari na maandalizi ya mustakabali wa mwisho wa mwanadamu.

Kwa mtazamo wa kijamii na kimaadili, maisha ya binadamu yanaweza kugawanywa katika hatua mbalimbali za umri, kuanzia utoto, ujana, utu uzima hadi uzee wa mwisho. Kila kundi la umri lina changamoto, fursa na wajibu wake.

Hatua za juu za umri, kuanzia miaka ya tisini na kuendelea, hufananishwa na machweo ya maisha, ambako binadamu hutakiwa kuangalia nyuma na kutathmini safari yake.

Umri wa kati, kuanzia miaka ya arobaini hadi sitini, ni kipindi cha maamuzi, mafanikio na marekebisho, wakati ambapo athari za maamuzi ya awali huanza kuonekana wazi.

Aidha,umri wa ujana na makuzi, kwa upande mwingine, ni msingi wa kujenga ndoto, maadili na mwelekeo wa maisha. Tazama mtiririko ufuatavyo;

1:Umri wa Ziada

1926 – Miaka 100

1927 – Miaka 99

1928 – Miaka 98

1929 – Miaka 97

1930 – Miaka 96

1931 – Miaka 95

1932 – Miaka 94

2:Umri wa Machweo

1933 – Miaka 93

1934 – Miaka 92

1935 – Miaka 91

1936 – Miaka 90

1937 – Miaka 89

1938 – Miaka 88

1939 – Miaka 87

1940 – Miaka 86

1941 – Miaka 85

1942 – Miaka 84

1943 – Miaka 83

1944 – Miaka 82

1945 – Miaka 81

1946 – Miaka 80

1947 – Miaka 79

1948 – Miaka 78

1949 – Miaka 77

1950 – Miaka 76

1951 – Miaka 75

3:Uzee

1952 – Miaka 74

1953 – Miaka 73

1954 – Miaka 72

1955 – Miaka 71

1956 – Miaka 70

1957 – Miaka 69

1958 – Miaka 68

1959 – Miaka 67

1960 – Miaka 66

1961 – Miaka 65

1962 – Miaka 64

1963 – Miaka 63

4:Umri wa Marekebisho na Maridhiano

1964 – Miaka 62

1965 – Miaka 61

1966 – Miaka 60

1967 – Miaka 59

1968 – Miaka 58

1969 – Miaka 57

1970 – Miaka 56

1971 – Miaka 55

1972 – Miaka 54

1973 – Miaka 53

5:Umri wa Mafanikio na Utimilifu

1974 – Miaka 52

1975 – Miaka 51

1976 – Miaka 50

1977 – Miaka 49

1978 – Miaka 48

1979 – Miaka 47

1980 – Miaka 46

1981 – Miaka 45

1982 – Miaka 44

1983 – Miaka 43

6:Umri wa Kufanya Maamuzi

1984 – Miaka 42

1985 – Miaka 41

1986 – Miaka 40

1987 – Miaka 39

1988 – Miaka 38

1989 – Miaka 37

1990 – Miaka 36

1991 – Miaka 35

1992 – Miaka 34

1993 – Miaka 33

7:Umri wa Kujitoa na Dhamira

1994 – Miaka 32

1995 – Miaka 31

1996 – Miaka 30

1997 – Miaka 29

1998 – Miaka 28

1999 – Miaka 27

2000 – Miaka 26

2001 – Miaka 25

2002 – Miaka 24

2003 – Miaka 23

8:Umri wa Ujana na Masomo

2004 – Miaka 22

2005 – Miaka 21

2006 – Miaka 20

2007 – Miaka 19

2008 – Miaka 18

2009 – Miaka 17

2010 – Miaka 16

2011 – Miaka 15

2012 – Miaka 14

2013 – Miaka 13

9:Umri wa Uangalizi wa Watoto Wachanga na Wadogo

2014 – Miaka 12

2015 – Miaka 11

2016 – Miaka 10

2017 – Miaka 9

2018 – Miaka 8

2019 – Miaka 7

2020 – Miaka 6

2021 – Miaka 5

2022 – Miaka 4

2023 – Miaka 3

2024 – Miaka 2

2025 – Mwaka 1

Hata hivyo, ujumbe mkubwa unabaki kuwa mmoja kwamba,hakuna aliye mdogo wala mkubwa kiasi cha kupuuza wajibu wa maisha.

Jamii inakumbushwa kuepuka kujidanganya kuwa bado kuna muda mwingi wa kufanya yaliyo sahihi.

Kila siku inayopita humsogeza binadamu karibu na mwisho wake. Ni vyema kila mmoja ajiulize; Nimefanya nini cha maana kwa familia yangu, jamii na kwa Mungu?.

Je, mchango wangu unaacha alama gani kwa wengine?. Nifanye nini leo kabla ya kuchelewa?.

Kumbuka

Siku moja mtu atastaafu, siku moja nafasi yake itachukuliwa na mwingine, siku moja mali na hadhi vitapoteza maana.

Siku moja jina lake litatanguliwa na neno marehemu, na siku moja atasimama mbele ya Muumba wake kutoa hesabu ya matendo yake.

Hakuna cheo, mali, uzoefu wala umaarufu vitakavyosalia. Kitakachobaki ni matendo mema au mabaya.

Tuishi kwa unyenyekevu, kufanya mema, kuepuka uovu na kuishi kwa amani na watu wote.

Pia, ishi kwa kumpenda jirani, acha dhuluma, kuthamini maisha, na kumweka Muumba mbele ya mambo ya dunia.

Kwa hakika, dunia ni ya kupita, lakini athari ya matendo ya mtu ni ya kudumu.Binadamu hukumbukwa si kwa alichomiliki, bali kwa yale aliyoyatenda.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here