ARUSHA-Kasoko ya Ngorongoro ndilo shimo kubwa zaidi la volkano duniani ambalo halijavunjika (lipo kamili) likiwa na wanyamapori wa aina mbalimbali, Mara nyingi huitwa Bustani ya Edeni kwa kuwa eneo hilo lina mkusanyiko mkubwa wa wanyamapori barani Afrika, ni kasoko yenye ufahari wa kipekee ambapo uhai hustawi kwa uwiano wa kipekee na wa asili.
