Mfumo wa kidijitali wa utoaji wa vyeti vya uasili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) unatarajiwa kuanza kutumika rasmi Machi 2, 2026.
Akizungumza mkoani Mbeya wakati wa mafunzo kwa wasafirishaji wa bidhaa nje ya nchi, Makamu wa Rais Kilimo wa Chemba ya Taifa ya Biashara (TNCC), Swallah Swallah, amesema mfumo huo utaongeza uwazi, kasi na ufanisi kwa kupunguza urasimu na muda wa kusubiri, huku ukiimarisha ushindani wa wafanyabiashara katika masoko ya nje.
Amesema mfumo huo utapatikana kupitia tovuti ya tcp.tncc.or.tz, kwa lengo la kurahisisha na kuharakisha huduma za biashara za kimataifa nchini na kuhimiza wafanyabiashara kujisajili na kuwasilisha maombi yao mtandaoni ili kunufaika kikamilifu na huduma hiyo.
Amesema mfumo huo utapatikana kupitia tovuti ya tcp.tncc.or.tz, kwa lengo la kurahisisha na kuharakisha huduma za biashara za kimataifa nchini na kuhimiza wafanyabiashara kujisajili na kuwasilisha maombi yao mtandaoni ili kunufaika kikamilifu na huduma hiyo.Akizungumza kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gwakisa Mwaikenda amesema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha mfumo huo unaunganishwa kikamilifu na mifumo ya forodha ili kurahisisha uthibitishaji na kuharakisha mchakato wa usafirishaji.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


.jpeg)

.jpeg)













