Magazeti leo Machi 17,2026

Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) unaolenga kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi katika Manispaa ya Lindi mkoani Lindi.
Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi Dkt. Stanford Mwakatage ambapo amesema kuwa kwa upande wa miundombinu ya barabara, kilomita 5.3 zitajengwa kwa kiwango cha lami ambapo licha ya kupendezesha mji, wananchi pia wataweza kupata huduma za usafiri kwa urahisi.

Kuhusu ujenzi wa stendi ya kisasa pamoja na soko la kisasa, kiongozi huyo amesema kuwa miradi hiyo itabadilisha kabisa mandhari ya manispaa ya Lindi na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.

“Soko la kisasa linalojengwa litatumiwa na wafanyabiashara takribani 400 huku stendi mpya ikitarajiwa kupokea magari 80 kwa wakati mmoja na hii itakuza uchumi wetu na kuongeza mapato kwa manispaa yetu”, amesema Dkt. Mwakatege.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here