Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) unaolenga kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi katika Manispaa ya Lindi mkoani Lindi.
Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi Dkt. Stanford Mwakatage ambapo amesema kuwa kwa upande wa miundombinu ya barabara, kilomita 5.3 zitajengwa kwa kiwango cha lami ambapo licha ya kupendezesha mji, wananchi pia wataweza kupata huduma za usafiri kwa urahisi.
Kuhusu ujenzi wa stendi ya kisasa pamoja na soko la kisasa, kiongozi huyo amesema kuwa miradi hiyo itabadilisha kabisa mandhari ya manispaa ya Lindi na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo



























