Uzinduzi wa jukwaa jipya la kidijitali la biashara ya madini lijulikanalo kama Tellus Minerals B2B unatarajiwa kufungua fursa mpya za masoko ya kimataifa kwa wachimbaji wadogo na wa kati nchini Tanzania, kwa kuwaunganisha moja kwa moja na wanunuzi, wawekezaji na wadau wa sekta ya madini duniani.
Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Tellus Minerals B2B, Idrissa Songoro akizungumza jijini Dar es Salaam amesema, jukwaa hilo limeanzishwa kwa lengo la kuleta mabadiliko katika biashara ya madini duniani kwa kutoa mazingira ya wazi na huru ya kidijitali yanayowawezesha wadau kuthibitishwa na kuwasiliana moja kwa moja bila kupitia kwa madalali.
Alieleza kuwa, kupitia mfumo huo, wachimbaji na wazalishaji wa madini wanaweza kuunganishwa moja kwa moja na wanunuzi wa kimataifa pamoja na wawekezaji, jambo litakalowawezesha kufanya majadiliano ya kibiashara kwa uwazi na kujenga ushirikiano endelevu.Soma kwa kina hapa》》》
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


























