WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo Kata ya Msongola katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia kwa kupigwa na radi wakiwa katika mazingira ya shule wakicheza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyothibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, tukio hilo limetokea Jumatano, Machi 18, 2026, wakati wanafunzi hao walipokuwa wakicheza katika eneo la shule.
Kamanda Muliro amesema kuwa, jumla ya wanafunzi watano walikumbwa na mkasa huo, ambapo watatu walipoteza maisha papo hapo, huku wawili wakijeruhiwa na kupelekwa hospitalini kwa matibabu.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

























