DAR-Wafanyakazi wanawake wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wameshiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi. 

Ushiriki wao umehusisha wafanyakazi kutoka Makao Makuu ya Benki Kuu jijini Dodoma, Ofisi Ndogo za Makao Makuu zilizopo Zanzibar na Dar es Salaam, pamoja na Matawi ya Benki Kuu ya Tanzania yaliyopo Mwanza, Mbeya, Arusha na Mtwara, sambamba na Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania.
Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kauli mbiu isemayo “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi Kufikia Dira 2050.”
Kupitia maadhimisho hayo, wanawake hao wameonesha mshikamano na uwajibikaji kwa jamii kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo utoaji wa misaada kwa makundi yenye uhitaji maalum katika jamii, kama sehemu ya kuendeleza utu, mshikamano na kuchangia ustawi wa jamii.









