DAR-Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amewataka Viongozi wa Vyama vya Michezo kujitathmini kuhusu uwazi wao katika kuendesha taasisi zao.
Makonda alisema hayo Machi 13, 2026, wakati akifunga Mkutano wa Baraza la Michezo la Taifa na Viongozi wa Vyama vya Michezo Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Amesisitiza kuwa, viongozi hao wana jukumu la kuwajibika kwa wanachama na kwa maendeleo ya michezo nchini na kuonya kuwa chama ambacho kitakuwa na matokeo mabaya, kiongozi wake hatakiwi kuendelea kuongoza.
Amehimiza viongozi hao kuimarisha uwazi na kushughulikia migogoro ya ndani inayokwamisha maendeleo ya michezo na kubainisha kuwa, wizara itafuatilia vyama hivyo.










