Waziri Makonda abisha hodi vyama vya michezo,wababaishaji kwaheri

DAR-Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, amewataka Viongozi wa Vyama vya Michezo kujitathmini kuhusu uwazi wao katika kuendesha taasisi zao.
Makonda alisema hayo Machi 13, 2026, wakati akifunga Mkutano wa Baraza la Michezo la Taifa na Viongozi wa Vyama vya Michezo Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Amesisitiza kuwa, viongozi hao wana jukumu la kuwajibika kwa wanachama na kwa maendeleo ya michezo nchini na kuonya kuwa chama ambacho kitakuwa na matokeo mabaya, kiongozi wake hatakiwi kuendelea kuongoza.

Amehimiza viongozi hao kuimarisha uwazi na kushughulikia migogoro ya ndani inayokwamisha maendeleo ya michezo na kubainisha kuwa, wizara itafuatilia vyama hivyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here