DAR-Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amefanya kikao na ujumbe kutoka Taasisi ya Koenig&Bauer yenye makazi yake nchini Uswisi, inayojihusisha na masuala ya fedha, ukiongozwa na Mkurugenzi wake wa Kanda ya Afrika, Bw. Jan Quitmeyer, kikao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha zilizoko Mtaa wa Madaraka jijini Dar es Salaam.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Washauri wakuu wa Taasisi hiyo, Bi. Sorah Thomhnair na Bw. Ronald Rwankangi pamoja na Kaimu Kamishna wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha Bi. Dionisia Mjema na Katibu wa Waziri wa Fedha Bw. Abeid Mzee.



