Waziri wa Fedha ateta na Wakurugenzi wa Standard and Poor's

DAR-Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) amekutana kwa mazungumzo na uongozi wa Kampuni ya Standard and Poor’s (S&P) inayojihusisha na kufanya tathmini ya uwezo wa nchi kukopesheka na kuyafikia Masoko ya Mitaji ya Kimataifa.
Ujumbe huo uliongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wake wa Kanda ya Afrika-nchini Afrika Kusini, Bi. Samira Mensah, akiambatana na Mkurugenzi Mshirika wa masuala ya biashara Idara ya Afrika wa taasisi hiyo, Bw. Raiston Muller, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, iliyoko Mtaa wa Madaraka jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine, mazungumzo yalijikita namna ya kufanya kazi na Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here