WASHINGTON D.C-Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, ameongoza kikao cha kujadili miradi ya kipaumbele ya Serikali katika sekta mbalimbali itakayofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Mzunguko wa 21 wa IDA (IDA-21 Cycle).
Kikao hicho kilichowahusisha Tume ya Taifa ya Mipango ikiongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Dkt. Tausi Kida, kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani pembezoni mwa Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayoendelea jijini Washington DC.



