Madereva wa IT waonywa kupakia abiria

PWANI-Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Salim Morcase tarehe 07 Aprili, 2026 amekemea vikali tabia ya madereva wa magari yanayosafirishwa kwenda nchi jirani (IT) kupakia abiria kwenye magari hayo kwani ni kinyume na sheria.
Akizungumza madereva hao Aprili 07, 2026 katika kituo cha Polisi Chalinze Kamanda Morcase ameeleza kuwa, magari hayo hayana usajili na hayaruhusiwi kupakia abiria kutoka sehemu moja kwenda nyingine hivyo hatakua na muhali kuchukua hatua kwa dereva yeyote wa IT atakayekamatwa amepakia abiria.

Aidha, amewataka madereva hao kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani, ikiwa ni pamoja na kujali usalama wao na watumiaji wengine wa barabara.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani litaendelea kufanya doria na ukaguzi wa mara kwa mara ili kudhibiti vitendo hivyo, na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kukiuka sheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here