Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) imetoa wito kwa Watanzania kushiriki katika uchangiaji wa ujenzi wa jengo la huduma za matibabu ya moyo. Kiasi cha shilingi bilioni 25 kinahitajika kukamilisha mradi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 9, 2026 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa KCMC, Profesa Gileard Masenga, amesema gharama za ujenzi pamoja na ununuzi wa vifaa tiba na vifaa vya hospitali zinakadiriwa kufikia jumla ya shilingi bilioni 25.
Ameeleza kuwa wataalamu watakaohudumia kitengo hicho tayari wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi, ikiwemo India, kwa ufadhili wa taasisi ya Global Heartcare Foundation.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo

































