Magazeti leo Aprili 10,2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) imetoa wito kwa Watanzania kushiriki katika uchangiaji wa ujenzi wa jengo la huduma za matibabu ya moyo. Kiasi cha shilingi bilioni 25 kinahitajika kukamilisha mradi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 9, 2026 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa KCMC, Profesa Gileard Masenga, amesema gharama za ujenzi pamoja na ununuzi wa vifaa tiba na vifaa vya hospitali zinakadiriwa kufikia jumla ya shilingi bilioni 25.

Ameeleza kuwa wataalamu watakaohudumia kitengo hicho tayari wamepata mafunzo ndani na nje ya nchi, ikiwemo India, kwa ufadhili wa taasisi ya Global Heartcare Foundation.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here