Makamu Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Uhamiaji, Said Abeid Kamugisha, amewataka waendeshaji wa mchakato wa usaili wa Ajira serikalini kutanguliza maslahi ya Taifa kwa kuzingatia uadilifu, uwajibikaji na uaminifu katika zoezi la kuwachuja waombaji kazi.
Wito huo umetolewa Aprili 13, 2026, jijini Arusha wakati wa kikao kazi kilicholenga kutoa mwongozo wa uendeshaji wa usaili kwa Vijana walioitwa kwenye usaili kinachofanyika katika Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA).
Kamugisha amesisitiza kuwa wataalamu kutoka kada mbalimbali wanapaswa kufanya maamuzi sahihi bila upendeleo wowote, ili kupata watumishi wenye sifa stahiki watakaosaidia kulijenga Taifa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo















