WASHINGTON D.C-Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ambaye pia ni Gavana wa Bodi ya Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, ameshiriki Mkutano wa nchi za Kundi la Kwanza za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency) wa Shirika hilo, uliofanyika katika Ofisi za Shirika hilo jijini Washington D.C, nchini Marekani, akiwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, katika mikutano inayoendelea ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, jijini humo.
Mkutano huo ulijadili Ripoti ya Muda ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Afrika kwa mwaka 2026, na namna ya Kukabiliana na Changamoto za Sekta ya Nje katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) kwa kutumia Mfumo Jumuishi wa Sera wa IMF (IPF).










