NA GODFREY NNKO
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeshiriki katika Soko la Jumla la Fedha za Kigeni (IFEM) na kuuza dola milioni 20 za Marekani kupitia mnada wa ushindani.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Mei 26,2026 na Kurugenzi ya Masoko ya Fedha ya BoT.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo,ushiriki wa BoT ni kwa majibu wa Sera yake ya ushiriki katika Soko la Fedha za Kigeni ya Mwaka 2023.
BoT kupitia mnada huo imeuza dola hizo kwa kiwango cha wastani cha kubadilisha fedha za kigeni cha Shilingi 2,619.31 kwa dola moja ya Marekani.
Lengo la mnada huo ni kuongeza ukwasi katika soko la fedha za kigeni ambapo benki 21 zimeshiriki na zikashinda zote.

