Mkuu wa Kamandi ya Vikosi Chini ya Makao Makuu ya Jeshi, Meja Jenerali Iddi Said Nkambi kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda akipokea Bendera ya Taifa kutoka Kikundi cha Tanzania kinachojumuisha Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto, Wizara na Taasisi za Kiraia walioshiriki zoezi la 14 la pamoja la vituo vya Uamrishaji vya Kijeshi vya Jumuiya ya Afrika Mashariki - Ushirikiano Imara 2026, Jijini Nairobi katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Brigedi 303 KV, Monduli-Arusha.





