DAR-Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam kupitia kwa Polisi Kata ya Bunju, Mkaguzi wa Polisi (INSP) Mwanamosi, limeendesha kampeni maalum ya kutoa elimu ya usalama kwa watoto 22, inayolenga kupiga vita vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuwajengea uwezo wa kujilinda dhidi ya mbinu mpya za wahalifu.
Mafunzo hayo ya ana kwa ana yamefanyika Mei 30,2026, katika eneo la Sobibo lililopo Mtaa wa Bunju A, Wilaya ya Kawe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mkakati endelevu wa kusogeza misingi ya ushirikishwaji wa jamii kwa tabaka la watoto.
Aidha,katika mafunzo hayo, INSP Mwanamosi aliwatahadharisha watoto hao vikali kutokubali kupokea zawadi au peremende kutoka kwa watu wasiowafahamu, huku akiwataka kuvunja ukimya na kutoa taarifa mapema kwa wazazi au Polisi pindi wanapohisi kufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia au kuona viashiria vyovyote vya hatari.
Mafunzo hayo yalihitimishwa kwa watoto hao kukumbushwa kuwa na nidhamu kwa wazazi, huku zoezi zima likiacha alama chanya ya ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na jamii, huku kukiwa hakuna changamoto wala matishio yoyote yaliyojitokeza kwenye himaya hiyo.
