Bodi ya Wakurugenzi ya BoT yafanya mazungumzo na Waziri wa Fedha

DODOMA-Bodi ya Wakurugenzi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye pia ni Gavana wa Benki Kuu, Bw. Emmanuel Tutuba, leo tarehe 18 Juni 2026 imemtembelea Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), jijini Dodoma na kufanya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa majukumu ya Benki Kuu.
Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Balozi Omar amesisitiza kuwa,Benki Kuu ina nafasi muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kwa kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji, ukuaji wa sekta binafsi, pamoja na maendeleo jumuishi ya uchumi.
Aidha, ameipongeza Benki Kuu kwa usimamizi thabiti wa sekta ya fedha, hususan benki za biashara, hatua iliyochangia kupungua kwa kiwango cha mikopo chechefu hadi kufikia chini ya asilimia 5.

Pamoja na pongezi hizo, alihimiza Benki Kuu kuendelea kufanya maboresho na mageuzi zaidi katika sekta ya fedha ili kuongeza mchango wake katika kukuza uchumi wa Taifa.
Kwa upande wake, Gavana Tutuba alieleza kuwa Benki Kuu itaendelea kutekeleza kwa uthabiti sera ya fedha, pamoja na kudhibiti mfumuko wa bei, ili kuhakikisha uwepo wa mazingira wezeshi ya ukuaji endelevu wa uchumi wa nchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here