BoT yaidhinisha mabadiliko ya jina la Habib African Bank Limited kuwa Africa and Gulf Bank (Tanzania) Limited

NA DIRAMAKINI

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeidhinisha rasmi mabadiliko ya jina la Habib African Bank Limited na kuanza kuitwa Africa & Gulf Bank (Tanzania) Limited, hatua inayokuja kufuatia mabadiliko katika umiliki wa hisa wa taasisi hiyo ya kifedha.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na BoT leo Juni 2,2026 mabadiliko hayo yameanza kutekelezwa rasmi kuanzia Mei 19, 2026, baada ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria na udhibiti zinazohitajika katika sekta ya fedha nchini.

Taarifa hiyo, iliyosainiwa na Naibu Gavana wa Benki Kuu anayeshughulikia Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Sauda K. Msemo imeeleza kuwa,hatua hiyo imechukuliwa kufuatia mabadiliko ya umiliki wa hisa katika benki hiyo, jambo lililopelekea kubadilishwa kwa utambulisho wa taasisi hiyo katika soko la huduma za kifedha.

Licha ya mabadiliko ya jina, makao makuu ya benki hiyo yataendelea kubaki katika eneo lilelile lililopo katika viwanja namba 813/23 na 814/23, kwenye makutano ya Barabara za Zanaki na Indira Gandhi katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here