Jaji Kiongozi awaapisha Naibu Wasajili 31 wapya wa Mahakama ya Tanzania

NA FAUSTINE KAPAMA
Mahakama

JAJI Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, leo tarehe 17 Juni, 2026 amewaapisha Naibu Wasajili 31 wapya wa Mahakama ya Tanzania aliowateua hivi karibuni.
Mhe. Agnes Lawrence Mchome.

Hafla ya uapisho huo imefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama jijini Dodooma. Uapisho huo unafanya jumla ya Naibu Wasajili wanaohudumu katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani kufikia 108.

Viongozi mbalimbali wa Mahakama, akiwemo Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju, wamehudhuria hafla hiyo. Wengine ni Majaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Amir Mruma na Mhe. Biswalo Mganga, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya na Kaimu Mtendaji Mkuu na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Bw. Victor Kategere.
Mhe. Richard Eustace Kabate.
Mhe. Janeth Elias Masesa.
Mhe. Ushindi Solomon Swallo.
Mhe. Charles Tumaini Mnzava.
Mhe. Cleofas Frank Waane.
Mhe. Liad Mohamed Chamshama.
Mhe. Hassan Ahmed Makube.
Mhe. Mariam Bakari Lusewa.

Wengine ni Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe. George Herbert, Msajili wa Mahakama Kuu, Mhe. Chiganga Tengwa, Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni, Bi. Mary Shirima, Mtendaji wa Mahakama Kuu, Bw. Leonard Magacha na Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu, Mhe. Sundi Fimbo.

Viongozi wengine ni Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Mahakama, Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania, Naibu Wasajili, Watendaji wa Mahakama, Watumishi wa Mahakama na Tume ya Utumishi wa Mahakama, Wazazi, Wenza, ndugu na jamaa wa Naibu Wasajili wapya.

Walioapishwa kwenye hafla hiyo ni Mhe. Agnes Lawrence Mchome kutoka Makao Makuu ya Mahakama, Mhe. Richard Eustace Kabate kutoka Makao Makuu ya Mahakama, Mhe. Janeth Elias Masesa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, Mhe. Ushindi Solomon Swallo kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Mhe. Charles Tumaini Mnzava kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara.

Wengine ni Mhe. Cleofas Frank Waane kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita, Mhe. Liad Mohamed Chamshama kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe, Mhe. Hassan Ahmed Makube kutoka Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu, Mhe. Mariam Bakari Lusewa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara na Mhe. Joyce Josephat Mkhoi kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha.

Kwenye orodha wapo pia Mhe. Consolata Peter Singano kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi, Mhe. Glory Gabriel Mwakihaba kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Shinyanga, Mhe. Mkama Ally Abdallah kutoka Mahakama Hakimu Mkazi Moshi, Mhe. Allu Omary Nzowa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida na Mhe. Zabibu Abeid Mpangule kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma.

Wengine ni Mhe. Asha Hassani Waziri kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Songea, Mhe. Erick Robert Marley kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza, Mhe. John Calist Msafiri kutoka Mahakama ya Wilaya katika Kituo Jumuishi Temeke, Mhe. Geofrey Jeremia Mhini kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Mhe. Gway Kwaslema Sumaye kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi.
Mhe. Joyce Josephat Mkhoi.
Mhe. Consolata Peter Singano.
Mhe. Glory Gabriel Mwakihaba.
Mhe. Mkama Ally Abdallah.
Mhe. Allu Omary Nzowa.
Mhe. Zabibu Abeid Mpangule.
Mhe. Asha Hassani Waziri.
Mhe. Erick Robert Marley.
Mhe. John Calist Msafiri.
Mhe. Geofrey Jeremia Mhini.
Mhe. Gway Kwaslema Sumaye.
Mhe. Gabriel Patrick Ngaeje.
Mhe. Zawadi David Laizer.
Mhe. Martha Mahumbuga.
Mhe. Kisasila Malangwa Saguda.
Mhe. Erasto Jacobo Philly.
Mhe. Japheti Bwire Manyama.
Mhe. Is-Haq Bakari Kuppa.
Mhe. Samwel Obasi Josiah.
Mhe. Jasmini Abdul Athuman.
Mhe. Mwanaheri Kassim Rashid.
Mhe. Domician Denice Mlashani.(Picha na MARY GWERA na HALIMA MNETE-Mahakama, Dodoma).

Wapo pia Mhe. Gabriel Patrick Ngaeje kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora, Mhe. Zawadi David Laizer kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Martha Mahumbuga kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, Mhe. Kisasila Malangwa Saguda kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Sumbawanga na Mhe. Erasto Jacobo Philly kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Wengine ni Mhe. Japheti Bwire Manyama kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, Mhe. Is-Haq Bakari Kuppa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, Mhe. Samwel Obasi Josiah kutoka Mahakama ya Wilaya Malinyi, Mhe. Jasmini Abdul Athuman kutoka Mahakama ya Wilaya Siha, Mhe. Mwanaheri Kassim Rashid kutoka Mahakama Hakimu Mkazi Tanga na Mhe. Domician Denice Mlashani kutoka Makao Makuu ya Mahakama.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here