Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe amewataka watumishi wa afya nchini kuwa makini zaidi katika kipindi hiki cha tahadhari ya ugonjwa wa Ebola, kufuatia mlipuko uliojitokeza katika nchi jirani za Congo na Uganda ili kujikinga wao na kuwakinga wengine.

Dkt. Magembe amesema hayo Mei 31, 2026 wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera na Hospitali ya Manispaa ya Bukoba akihitimisha ziara yake ya kukagua hali ya utayari wa kujikinga na ugonjwa wa ebola usiingie nchini katika maeneo ya mipakani mkoani humo.
Dkt. Magembe amesema kuwa dalili za awali za Ebola kama homa, kuumwa kichwa, uchovu wa mwili, kutapika na kuharisha zinaweza kufanana na magonjwa mengine, hivyo wahudumu wa afya wanapaswa kuwa na umakini mkubwa wanapowahudumia wagonjwa na kuchukua tahadhari zote muhimu za kinga.













Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












