Magazeti leo Juni 17,2026

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ni kumbusho kwa jamii kuhusu wajibu wa kulinda na kuendeleza haki za watoto, sambamba na kumbukumbu ya watoto wa Soweto nchini Afrika Kusini waliopigania haki ya kupata elimu bora.
Akizungumza Juni 16, 2026 jijini Dodoma, Prof. Mkenda ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuiweka elimu miongoni mwa vipaumbele vyake, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amesisitiza kuwa kila mtoto wa Kitanzania lazima apate elimu.

Kwa msingi huo, Waziri Mkenda amesema Serikali imeweka mkazo katika kuhakikisha usawa na ujumuishi katika elimu kwa watoto wote, ikiwemo kuimarisha usawa wa kijinsia ili kila mtoto apate fursa ya kujifunza na kufikia ndoto zake.




























Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here