Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ni kumbusho kwa jamii kuhusu wajibu wa kulinda na kuendeleza haki za watoto, sambamba na kumbukumbu ya watoto wa Soweto nchini Afrika Kusini waliopigania haki ya kupata elimu bora.
Akizungumza Juni 16, 2026 jijini Dodoma, Prof. Mkenda ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuiweka elimu miongoni mwa vipaumbele vyake, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amesisitiza kuwa kila mtoto wa Kitanzania lazima apate elimu.
Kwa msingi huo, Waziri Mkenda amesema Serikali imeweka mkazo katika kuhakikisha usawa na ujumuishi katika elimu kwa watoto wote, ikiwemo kuimarisha usawa wa kijinsia ili kila mtoto apate fursa ya kujifunza na kufikia ndoto zake.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




































