Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua Awamu ya Pili ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia itakayofanyika Juni 20, 2026 katika Viwanja vya Dole, Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari Juni 17, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera, amesema kuwa kampeni hiyo ni utekelezaji wa maono na maelekezo ya Rais Samia ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za msaada wa kisheria na haki zao kwa wakati.Amesema kuwa kampeni hiyo ilianzishwa baada ya Rais Samia kubaini kuwa wananchi wengi wanakosa haki zao kutokana na kutofahamu sheria na kushindwa kupata msaada wa kisheria wanapokumbana na changamoto mbalimbali za kisheria.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


















