Serikali kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.
Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo






















