Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho, amesema kuwa sera ya ulinzi ni mhimili muhimu unaolinda usalama wa taifa na kuweka msingi imara wa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha uwezo wa taifa wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazojitokeza katika mazingira ya sasa ya dunia.
Dkt. Nyansaho ametoa kauli hiyo Aprili 4, 2026 alipowasilisha mhadhara wa kimkakati katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania (National Defence College – Tanzania) kilichopo Kunduchi, Dar es Salaam, kwa washiriki wa Kozi ya Kistrategia ya 14, chini ya mada “Umuhimu wa Sera ya Ulinzi katika Kuimarisha Usalama wa Taifa.”Katika mhadhara wake, Waziri Nyansaho ameeleza kuwa sera ya ulinzi si nyaraka za kawaida za serikali bali ni dira inayotoa mwongozo wa kimkakati katika kulinda mipaka, watu na rasilimali za taifa, huku ikihakikisha nchi inakuwa salama na yenye utulivu wa kutosha kuendeleza shughuli za maendeleo.
“Usalama wa taifa ni msingi wa maendeleo. Bila usalama, ustawi wa uchumi, uwekezaji na huduma za kijamii haviwezi kufikiwa kwa ufanisi unaotarajiwa,” amesisitiza Waziri Nyansaho.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














