Mawaziri wa Nishati kutoka nchi wanachama wa Soko la Pamoja la Nishati Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool-EAPP) wameazimia kuharakisha utekelezaji wa soko la pamoja la umeme ili kuimarisha upatikanaji wa nishati, kuongeza biashara ya umeme kati ya nchi wanachama na kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa umeme katika ukanda huo.
Azimio hilo limefikiwa wakati wa Mkutano wa 22 wa Baraza la Mawaziri wa EAPP uliofanyika Julai 9 hadi 10, 2026 jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo Tanzania iliwakilishwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb), kwa niaba ya Waziri wa Nishati.Mkutano huo uliwakutanisha Mawaziri wa Nishati, wakuu wa taasisi za umeme na wawakilishi wa sekta ya nishati kutoka nchi wanachama wa EAPP kujadili hatua za kuimarisha ushirikiano wa kikanda kupitia biashara ya umeme, uunganishaji wa gridi za taifa na matumizi bora ya rasilimali za nishati.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




















