Magazeti leo Julai 26,2026

Madereva wanaosafirisha makaa ya mawe nchini wamehimizwa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia usafirishaji wa kemikali na bidhaa hatarishi ili kulinda usalama wa wananchi, mazingira na mali, sambamba na kuhakikisha shughuli za usafirishaji zinafanyika kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa.
Wito huo umetolewa na Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Kusini, Dkt. Hadija Mwema wakati akifungua mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyowahusisha madereva wa malori yanayosafirisha makaa yamawe wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Meneja alisema kuwa pamoja na makaa ya mawe kuwa bidhaa muhimu katika shughuli za kiuchumi, usafirishaji wake unapaswa kufanyika kwa kuzingatia sheria na kanuni za Usimamizi na Udhibiti wa kemikali ilikuzuia ajali, uchafuzi wa mazingira na madhara yanayoweza kujitokeza wakati wausafirishaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here