ZANZIBAR-Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mheshimiwa Hamza S.Johari ameshiriki katika ufunguzi wa Semina Elekezi ya Mawaziri,Naibu Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Mawasiliano Serikalini katika Ikulu ya Tunguu,Zanzibar.
Semina hiyo ya siku mbili imefunguliwa Julai 28,2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo amesisitiza kuwa,mawasiliano ni sehemu ya uongozi na nyenzo ya kimkakati ya kulinda maslahi ya Taifa.


