KILIMANJARO-Julai 2,2026 Mahakama ya Wilaya ya Siha mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo,Mhe.Elibahati Petro imemkuta na hatia mshtakiwa wa shauri la jinai namba 13773/2026,Bw.Ismael Siroiya Pallangyo ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Makiwaru B kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Siha.
Mshtakiwa ametiwa hatiani kwa kosa la kupokea hongo ya shilingi 20,000 kutoka kwa mwananchi ili asimfikishe kwenye vyombo vya sheria kwa kumshambulia askari mgambo.
Kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya mwaka 2023.
Mshtakiwa baada ya kutiwa hatiani aliomba kupunguziwa adhabu,ambapo Mahakama iliamuru mshtakiwa kulipa faini ya shilingi 500,000 au kutumikia kifungo cha miaka mitatu gerezani.
Aidha,mshtakiwa amelipa faini ya shilingi 500,000 na kukatiwa stakabadhi ya Serikali na yupo huru.
Tags
Habari
Mahakamani Leo
Rushwa ni Adui wa Haki
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)
