Gavana Tutuba afanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi mpya wa IMF nchini Tanzania

DODOMA-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi Mpya wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) nchini Tanzania, Bi. Jana Bricco, katika Makao Makuu ya Benki Kuu jijini Dodoma, tarehe 26 Agosti 2026.
Katika kikao hicho, Gavana Tutuba alieleza hatua mbalimbali zinazoendelea kutekelezwa na Benki Kuu katika kusimamia ukuaji na ustahimilivu wa uchumi, ikiwemo kuimarisha uthabiti wa thamani ya Shilingi, kuongeza akiba ya fedha za kigeni kupitia programu ya ununuzi wa dhahabu, pamoja na kuongeza upatikanaji wa huduma jumuishi za fedha.
Kwa upande wake, Bi. Bricco aliipongeza Tanzania kwa kukamilisha programu mbili za kifedha za IMF, ambazo ni Extended Credit Facility (ECF), inayolenga kusaidia nchi kuimarisha uchumi kupitia upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu, na Resilience and Sustainability Facility (RSF), inayosaidia kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha ustahimilivu wa uchumi. Programu hizo zimeiwezesha Tanzania kupata jumla ya Dola za Marekani milioni 443.9.
Akihitimisha kikao hicho, Gavana Tutuba aliahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Benki Kuu na IMF, hususan katika kuendeleza sera na hatua zinazolenga kudumisha uthabiti wa uchumi na kukuza maendeleo endelevu nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here