MOROGORO-Mahakama ya Wilaya ya Kilombero imemhukumu Isaya Joel Ndemo kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la ubakaji katika shauri la jinai namba MLB/IR/788/2025, lililohusisha tukio lililotokea tarehe 21 Novemba 2025 majira ya saa 06:00 asubuhi.
Kwa mujibu wa taarifa za shauri hilo, mtuhumiwa alidaiwa kumvizia mlalamikaji akiwa shambani, kisha kumkaba shingoni na kumfanyia kitendo cha ubakaji.Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alikamatwa na kufikishwa katika kituo cha Polisi kwa ajili ya mahojiano na hatua zaidi za kisheria.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa Mahakama ya Wilaya ya Kilombero tarehe 05 Januari 2026 ambapo shauri hilo liliendelea kusikilizwa na upande wa mashtaka kuwasilisha ushahidi. Baada ya kusikiliza na kupitia ushahidi uliowasilishwa, mahakama ilimtia hatiani kwa kosa hilo na kutoa hukumu tarehe 19 Agosti 2026.
Katika hukumu hiyo, Mahakama ya Wilaya ya Kilombero imemwamuru Isaya Joel Ndemo kutumikia kifungo cha miaka 30 gerezani pamoja na kulipa fidia ya shilingi 500,000 kwa mlalamikaji.