DAR-Jumuiya ya Kifalme ya Afrika imepongeza uamuzi wa Serikali ya Tanzania wa kuwashirikisha wataalamu wa sheria na majaji kutoka nchi nyingine za Afrika katika Tume ya Uchunguzi wa Kijinai inayochunguza matukio ya vurugu na uhalifu yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025.
Katika tamko lake la tarehe 11 Agosti 2026, Jumuiya hiyo imesema hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha uwazi, weledi, uadilifu na imani ya wananchi katika mchakato wa uchunguzi.
Katika tamko lake la tarehe 11 Agosti 2026, Jumuiya hiyo imesema hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha uwazi, weledi, uadilifu na imani ya wananchi katika mchakato wa uchunguzi.Jumuiya imeeleza kuwa taasisi za kitaifa zinapokabiliana na masuala yenye umuhimu mkubwa kwa taifa, zinaweza kunufaika kutokana na uzoefu na utaalamu wa wataalamu kutoka mamlaka nyingine ndani ya Afrika.
Jumuiya hiyo imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, pamoja na Serikali yake kwa kufungua nafasi ya wataalamu kutoka nchi nyingine za Afrika kushiriki katika mchakato huo.
Kwa mujibu wa tamko hilo, ushiriki wa majaji kutoka nje ya Tanzania haupaswi kutafsiriwa kama ishara ya kutokuamini mfumo wa haki wa Tanzania.
Badala yake, Jumuiya imeona hatua hiyo kama ishara ya kujiamini, ukomavu wa taasisi na utayari wa kutumia mitazamo na uzoefu mbalimbali wa kisheria katika kushughulikia jambo lenye umuhimu mkubwa kitaifa.