NA DIRAMAKINI
DAWA za kulevya, ni sumu ya maisha,
Huvunja afya njema, na kuleta mateso;
Zinapora matumaini, na kufisha ndoto,
Kataa dawa hizo, chagua maisha bora.
Usikubali tamaa, ikupoteze njia,
Jiepushe na vishawishi, linda afya yako;
Ukitambua kosa, tafuta msaada,
Kwa moyo wa dhati, utaweza kupona.
Sema hapana, kwa dawa za kulevya,
Chagua maisha mema, timiza ndoto zako!.
Je,una taarifa kuhusu wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya? Kama ndiyo, piga simu bure kwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) namba 119, taarifa zitapokelewa kwa usiri mkubwa na kufanyiwa kazi kwa haraka.
Tags
DCEA
DCEA Tanzania
Habari
Kataa Dawa za Kulevya na Timiza Ndoto Zako
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)
