RUVUMA-Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amekutana na kufanya mazungumzo na Kamanda wa Brigedi ya 401 Kanda ya Kusini, Brigedia Jenerali Sijaona Michael Myala, ofisini kwake mjini Songea.
Katika mazungumzo hayo, RC Ahmed amesema usalama wa mkoa ni msingi wa uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla, hasa kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kimkakati inayoendelea katika mkoa na taifa.
Ameeleza matarajio ya viongozi wa mkoa kuwa Kamanda huyo ataendeleza ushirikiano wa karibu na vyombo vingine vya usalama katika kuimarisha ulinzi wa mipaka ya nchi. Akisisitiza kuwa nidhamu, ujasiri na utayari wa kioperesheni ni misingi muhimu ya brigedi hiyo.
Tags
Brigedi ya 401 Kanda ya Kusini
Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed
Brigedia Jenerali Sijaona Michael Myala
Habari
Kanda ya Kusini
Mkoa wa Ruvuma


