DAR-Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari,Agosti 4,2026 jijini Dar es Salaam, amekutana na Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Dkt.Martin Wilbert Kolikoli, kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji wa Baraza hilo.
Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Johari amesema kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inaendelea kupitia sheria mbalimbali za nchi kuwezesha utekelezaji wa Dira 2050 na kuongeza ufanisi katika utendaji na utoaji wa huduma.
Vilevile Mhe. Johari amesisitiza kwamba Masoko ya mtaji ni nyezo muhimu katika utekelezaji wa Dira 2050, hivyo ni muhimu sheria zake zikaendana na dira hiyo na kasi ya maendeleo ulimwenguni.
Kwa upande wake, Dkt. Kolikoli ameeleza majukumu ya Baraza la Masoko ya Mitaji pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake.
Pia amependekeza maboresho ya sheria zinazohusu masoko ya mitaji, dhamana na soko la bidhaa, hususan katika maeneo ya ulinzi wa haki na utatuzi wa migogoro.
Dkt. Kolikoli amemkabidhi Mhe. Johari jarida la CMT pamoja na kutoa wito kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kushirikiana na CMT katika kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya masoko ya mtaji.
Tags
Habari
Hamza Johari
Masoko ya Mitaji
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali







