DAR-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Catherine Karemu, tarehe 21 Agosti, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yamejikita katika kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, pamoja na kubainisha malengo ya pamoja katika kuendeleza ushirikiano wauwili katika yenye kuleta maendeleo yenye manufaa kwa wananchi wa mataifa yote mawili.



